Psalms 19:1-6

Utukufu Wa Mungu Katika Uumbaji

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 aMbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,
anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2 bSiku baada ya siku zinatoa habari,
usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3Hakuna msemo wala lugha,
ambapo sauti zao hazisikiki.
4 cSauti yao imeenea duniani pote,
nayo maneno yao yameenea
hadi miisho ya ulimwengu.

Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5 dlinafanana na bwana arusi
akitoka chumbani mwake,
kama shujaa afurahiavyo
kukamilisha kushindana kwake.
6 eHuchomoza upande mmoja wa mbingu,
na kufanya mzunguko wake
hadi upande mwingine.
Hakuna kilichojificha joto lake.
Copyright information for SwhNEN